NA DIRAMAKINI
WAENDESHA pikipiki maarufu bodaboda mkoani Mara wamefanya maandamano ya amani ya kulipongeza jeshi la Polisi mkoani humo kwa jitihada na jinsi linavyoendelea kukabiliana na vitendo vya kihalifu.



Ameliomba Jeshi la Polisi Mkoani Mara lisikatishwe tamaa na kauli za wanasiasa ambao wanaweza kutumia operesheni hizo kufanya upotoshaji kwa umma. Huku akisema kuwa waendesha bodaboda wataendelea kushirikiana na jeshi hilo kumaliza vitendo vya kihalifu kwa kutoa ushirikiano thabiti.
Ameongeza kuwa, jeshi hilo lisirudi nyuma kuwachukulia hatua wale wote wanaobainika kujihusisha na Vitendo vya kihalifu wakiwemo majambazi, vibaka kwani hatua hiyo itazidi kuwafanya wananchi waendelee na shughuli za uzalishaji mali kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Waendesha Boda boda Wilaya ya Musoma Mjini Stephano Silas amewataka waendesha boda boda Wilayani humo kujisajili katika vituo halali vya kazi. Na kwamba, boda boda wote wafuate sheria na taratibu za nchi pia wasijihusishe na vitendo vya kihalifu ambavyo vitawafanya watiwe hatiani.
Amesema wanaokuja kufanya kazi ya boda boda Wilayani Musoma na Mkoani Mara kwa ujumala, wahakikishe wanafanya kazi hiyo kihalali, lakini wanaokuja na kuingia katika kazi hiyo wakiwa na agenda ya kufanya uhalifu amesema hawatafanikiwa kutokana na ushirikiano wao na Jeshi la Polisi.

Kamanda Tibishubwamu amesema, Jeshi hilo litaendelea kuimarisha ulinzi na usalama kusudi wafanye kazi saa 24. Huku akiwaahidi ushirikiano boda boda wote na wananchi wote mkoani Mara ili wafanye kazi za uzalishaji mali kwa amani na utulivu.