NA FRESHA KINASA
SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Victoria Farming and Fishing Organization (VIFAFIO) lililopo Musoma mkoani Mara limezindua mradi wa kupinga ukatili wa kijinsia maeneo ya uvuvi katika kata nne za Halmashauri ya Wilaya ya Bunda mkoani Mara.

Uzinduzi huo umefanyika leo Septemba 27, 2022 makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bunda yaliyopo Kata ya Kibara wilayani humo na kuhudhuriwa na viongozi wa halmashauri hiyo, Kamati za Usimamizi wa Mialo (BMU), viongozi wa dini pamoja na Maafisa Watendaji wa kata zinazonufaika na mradi huo.
Pia, Septemba 22, 2022 shirika hilo lilizundua mradi huo katika kata saba za Halmashauri ya Wilaya ya Musoma. Ambapo utatekelezwa kwa kipindi cha miezi nane katika Halmashauri zote mbili kuanzia Septemba 2022, hadi Aprili 2023 katika halmashauri ya Wilaya ya Musoma na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda na utagharimu jumla ya shilingi milioni 37 kwa halmashauri zote.
Ambapo katika Halmashauri ya Wilaya ya Musoma mradi huo utatekelezwa katika kata saba ikiwemo kata ya Bukima, Rusoli, Bukumi,Nyamrandirira, Bwasi, Msanja na Kiriba.

Amesema kuwa, mradi huo waliomba kwa mfadhili utekelezwe kwa miaka mitatu kwa thamani ya zaidi ya Shilingi milioni 200 walizoomba lakini wamepewa shilingi milioni 37 watekeleze kwa kipindi cha miezi nane. Hivyo ameomba ushirikiano kutoka kwa viongozi wa maeneo husika ambayo mradi huo unatekelezwa ili uwe na tija kwa Jamii Kama.ivyokusudiwa.

Amesema, mradi huo unatarajia kuleta matokeo ikiwemo kuwafanya wanawake na watoto wachukue hatua kwa kuripoti vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa kwa mamlaka za serikali na Jamii iwe na uwezo wa kudhibiti vitendo vya ukatili wa kijinsia sambamba na kuimarisha mfumo bora katika kamati za Vijiji na kata zinazohusika na kupinga vitendo hivyo.

Ameongeza kwa kusema kwamba, Serikali inatambua kwa dhati mchango wa maendeleo unaofanywa na mashirika yasiyo ya Kiserikali Katika kuwasaidia wananchi na hivyo kuunga mkono juhudi za serikali kwa vitendo Wilayani humo.

Amesema kwamba, maeneo ya mialo katika Halmashauri ya Wilaya hiyo yanakabiliwa na tatizo hilo la ukatili wa kijinsia ikiwemo kata yake anayotoka ya Iramba hivyo kupitia mradi huo utawezesha kuleta mabadiliko chanya kwa jamii ya wavuvi.
Aidha Afisa Ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Bunda Fausta Parali amesema elimu ya kupinga ukatili wa Kijinsia itakayotolewa katika mialo wakati wa Mradi unatekelezwa iangazie elimu ya ulinzi, malezi na makuzi kwa watoto sambamba na kuhuisha na kutoa mafunzo kwa kamati za ulinzi na usalama wa Wanawake na watoto ili kudhibiti vitendo vya ukatili wa kimwili, kiuchumi, kisaikolojia na kiuchumi.

Padri Costantine ameihimiza Jamii iendelee kuwa na mahusiano mazuri na Watoto, Jamii ijengewe uwezo kujua haki za watoto sambamba na kutumia sanaa, michezo maonesho maeneo ya mialo kutoa elimu ya ukatili.