NA MWANDISHI WETU
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, amesema ushirikiano wa karibu unahitajika kati ya Serikali ya Zanzibar na Australia katika kuzitumia vyema fursa za kiuchumi zilizopo kama njia ya kuwakomboa kimaisha.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggDaKBb9plbjamNYm8wxWCpKrHMYqLQ4kX0Qnp24Z1z9HCBXK4TevUEsIxdpUshgn-s8-PJIUYITZHB7eP_naV2XJ2kGTpFsgd9Cc1_qwWQO0lHBp3u036B6rVy7MUhvPXSnQillq-IXJe0rbBeoYpzsKZ_nlWg49QGEfAsRN-9oycOZc5KCLKSvvFHQ/s16000/IMG-20220920-WA0024.jpg)
Amesema kuwa, yapo mambo yanayoshabihiana katika nchi hizo mbili na kwamba ushirikiano wa karibu ikiwemo kubadilishana ujuzi ni wa muhimu ili kuleta tija katika uzalishaji.
“Uchumi wa Buluu, uhifadhi wa mazingira ya bahari na ufugaji wa nyuki, ni maeneo muhimu sana ambayo ikipatikana nguvu ya mashirikiano, basi Zanzibar itapiga hatua katika kukamilisha azma ya serikali na kuzalisha ajira zaidi kwa wananchi,”amesisitiza Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Akielezea kuhusu ufugaji wa nyuki, Mhe. Othman amesema Zanzibar inazalisha asali nzuri sana ya nyuki wanaofugwa katika mikandaa ila kutokana na kukosekana kuitangaza na masoko ya uhakika basi fursa ya kipato inapungua.
“Tumeona zipo bidhaa nyingi ambazo zinazalishwa nchini kwetu, lakini kutokana na uhifadhi na namna duni ya kuzitangaza zinakosa masoko, ila ukizikuta namna zilivyohifadhiwa katika masoko makubwa kama ya nchi ya Dubai na kwengineko na zinavyokuwa na thamani kubwa zaidi, tunaona ni wazi ipo haja ya kuwa na mazingira mazuri ya elimu ya uhifadhi na kuzitangaza ili kulilinda soko letu la ndani.”
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXeydhc_06r0R5BLXJLk8W3EUk0u4HC2Cva1G1hH1hA_ZaXA9U-WgiAWKzj_bRaQOqAtU_3CooXq9hJ2sMr125T9Q1v3OOxny9FERQDj9IkjLJze-IS7-Y6Qq-bbOUNBRQPjGTljXOX-jKLSpzMKf4NGuNZHKTlN1llx8A7CBzIsh6nyo4SmB1IWeyyg/s16000/IMG-20220920-WA0025.jpg)
Aidha ameeleza kuwa jamii inapaswa kujiepusha na ukataji miti kiholela na badala yake kujikita kupanda miti na kuhifadhi mazingira hasa ya fukwe ili kuepusha tatizo hilo.
Aidha, Mheshimiwa Othman amesema taasisi zinazohusika na utamaduni hazina budi kuhakikisha wanautangaza utamaduni wa nchi kwa kupitia matamsha makubwa ya kimataifa ili kuitumia fursa hio kuitangaza nchi na utamaduni wake, sambamba na kumuomba Balozi wa Australia kuangalia namna na kuisaidia Zanzibar katika hilo.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjQOXkiJY5TvFHTmNMYzHcTstvdTQMPVu5o_qF49BAFDDSyNKx90pbqOItjKPyJg_d5hR8JNJGQS0VJNW0kpbHH5fTEmREqkhEap0XBp__XMg2o7lA-mojqhul7Gd-jJ8vXchPhfSfH4EUzg7sJBAG_ZJtw7P7W3pVUAI8rwPidNK7jDHygGUMuXKPefw/s16000/IMG-20220920-WA0027.jpg)
Katika ujumbe wake, Balozi Luke ameambatana na Mke wake, Bi. Hellen Luke, na msaidizi wake, Bw. Lewisi Hirst.