NA DIRAMAKINI
LEO Septemba 30, 2022 wadau mbalimbali wameshiriki mjadala muhimu na maalum wa Kitaifa ambao uliangazia juu ya usalama nchini na operesheni mbalimbali za Jeshi la Polisi.

SACP. DAVID MISIME, MSEMAJI WA JESHI LA POLISI
"Majukumu makubwa ya Jeshi la Polisi ni kulinda maisha ya watu na mali zao pia kukamata, kupeleleza na kuwafikisha watuhumiwa mahakamani, haya yote huwezekana kutokana operesheni mbalimbali kupitia doria baada ya kupata taarifa za watuhumiwa kutaka kufanya matukio mbalimbali.
"Matukio ya kiuhalifu mara nyingi hutokea mitaani ambako kuna makazi ya watu, hivyo Jeshi la Polisi limekuwa na utaratibu wa kutoa elimu kwa wananchi namna ya kuwatambua wahalifu mbalimbali katika maeneo yao na hasa kwa watu wasiowatambua wakizunguka na kuzurura bila utaratibu na kuonesha ishara ya mashaka.


ZUBERI S. CHEMBERA, NAIBU MKURUGENZI WA UPELELEZI WA MAKOSA YA JINAI ZANZIBAR


"Diplomatic Polisi ni kikosi kazi chenye mchanganyo wa askari wote au vyombo vyote vya ulinzi na usalama katika visiwa vya Zanzibar, lengo likiwa kuunganisha nguvu kusudi kila rasilimali tuliyonayo tunaitumia ili kuhakikisha ulinzi na usalama unataradadi Zanzibar.
"Zanzibar imezungukwa na maji katika pembe zake zote, hivyo moja ya mkakati ni kuhakikisha tunashirikiana na mikoa yote ya mwambao wa Hindi unayotuzunguka kama Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Lindi na Mtwara hivyo tumekuwa tukifanya vikao na operesheni mbalimbali kuhakikisha usalama wa wananchi,"amesema.
RPC. LONGINUS A. TIBISHUBWAMU, KAMANDA WA POLISI MKOA WA MARA



BISHOP BENSON BAGONZA, ASKOFU WA KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI TANZANIA (KKKT)

"Taasisi nyingi sana siku hizi zimeingiliwa na makanjanja hata makanisani, misikitini, vyombo vya dola, wanasiasa kote makanjanja wapo wengi sana ambao wanapotosha ukweli kwa maslahi yao binafsi,"amesema.
WAMBURA IGEMBYA, KATIBU WA UVCCM MKOA WA MARA
"Niwaombe wanasiasa kutokujihusisha kwa namna yeyote ya kufurahishwa na uhalifu unaoendelea katika maeneo yetu tuwape ushirikiano wa kutosha Jeshi la Polisi katika kuwavumbua wahalifu katika maeneo yetu kusudi taifa liwe na amani na utulivu.
"Ulinzi shirikishi ni jambo jema sana kukiwa na ushirikishwaji kwa wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama nchi yetu itakuwa tulivu na ninauhakika uhalifu utapungua kama sio kuisha kabisa,"amesema.