NA FRESHA KINASA
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Balozi Dkt.Pindi Chana amesema, wizara hiyo inaendea kutangaza vivutio na maeneo mbalimbali ya utalii nchini kupitia njia mbalimbali ikiwemo michezo, mikusanyiko na matamasha katika kuhakikisha kwamba taifa linapiga hatua kimaendeleo kupitia utalii wa ndani na utalii wa wageni kutoka mataifa mbalimbali wanaokuja nchini.

Mbio hizo zilikuwa katika makundi ya kilomita nne, kilomita13 na kilomita 22 ambapo kauli mbiu ya ilikuwa inasema 'Talii Kiutamaduni', jenga na piga hela' ambapo Waziri Chana na Naibu Waziri wa wizara hiyo pamoja n viongozi mbalimbali wa Wizara na Serikali wameweza kushiriki mbio hizo.

Ameongeza kuwa, sekta ya utalii nchini ina umuhimu mkubwa katika kuleta maendeleo kwa watanzania, hivyo wizara hiyo itaendelea kutekeleza majumumu yake kwa ufanisi katika kuhakikisha maeneo na vivutio vyote vinatangazwa kwa ufanisi kuvuta watalii wa ndani na watalii wa nje kuja nchini.


Amesema, mbio hizo zimeadhimisha kuzaliwa kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa vitendo na kwamba kitendo hicho ni muhimu sana. Huku akisema kumbukumbu hizo zitazidi kuenziwa kwa faida ya Watanzania.

Ameongeza kuwa, Watanzania wanapaswa kukumbuka kwamba maisha, utumishi na upekee wa Mwalimu Nyerere ni mojawapo ya urithi mkubwa wenye thamani kwa taifa, Afrika na Dunia kwa ujumla.

Pia, mbio hizo za Mwalimu Nyerere ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango wa miaka 10 ya kuenzi na kutangaza urithi wa Mwalimu Nyerere uliozinduliwa na Waziri Mkuu mstaafu Mheshimiwa Mizengo Pinda tarehe 13, Aprili 2022 wilayani Butiama mkoani Mara wakati wa sherehe ya miaka 100 ya Mwalimu Nyerere.

"Kilomita za kukimbia zimegawanyika kulingana na tarehe, mwezi aliozaliwa yaani tarehe 13,04, 1922 wapo waliokimbia kilomita 13 hiyo ni tarehe aliyozaliwa, wapo waliokimbia kilomita 4 huo ni mwezi aliozaliwa, wapo waliokimbia kilomita 22 hiyo ni kumbukumbu mwaka aliozaliwa,"amesema Dkt.Masebo.

Aidha, amewataka Watanzania kutambua kwamba Makumbusho ya Taifa imebeba na inashughulika na historia ya Tanzania na mahusiano ya Tanzania na Jamii za nje ya Tanzania, inashughulika na Utamaduni wa Taifa, inashughulika na ujenzi wa misingi ya taifa, kutunza na kilinda utamaduni, usalama kama nchi, hatima ya ustawi wa taifa, utamaduni wa Taifa, utaifa wetu, kumbukumbu zote zinazolinda taifa.

Neema Peter ni mkazi wa Butiama amesema kuwa, Mwalimu Nyerere alikuwa kiongozi bora na mnyenyekevu aliyetanguliza mbele uzalendo, uadilifu na uwajibikaji.
Aidha,ameshauri Watanzania wote kuzidi kuenzi falsafa zake na kuyaishi mema yote katika kumuenzi kwa vitendo.
Tags
Habari
Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere
Maliasili na Utalii
Miaka 100 ya Mwalimu Nyerere
Michezo