NA DIRAMAKINI
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, amesema mlipuko wa maradhi ya surua ni tatizo la Ulimwengu wote, bali kinachohitajika ni taarifa sahihi, uelewa, na tahadhari kwa kila upande.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhd0C-zXbSI_1KJg7FSoofz7wuj0sDi1LVWV2PLXWhJyu0evTe525B18hyaz-z0WdpcD2IGpvZPGfWBmgruWa2jzYmSJxyaub92NZokhEzjnBa5VW7UO2it8V0ZX-G1SuFatUePouVwZTd3ApIOBiOMTpNG7u4H1bbXOCWhOJGlcBx3KaclQETa-v1BQA/s16000/IMG-20221029-WA0056.jpg)
Amesema kuwa, kimantiki kasi ya maambukizo ya Surua hapa Visiwani inaonekana ni kubwa, kwa kuzingatia uhaba wa raslimali na maandalizi duni ya kukabiliana na janga hilo, bali si vyema kukuza taarifa za uwepo wa maradhi hayo, kwa nia ya kuwatishia wageni na wale wanaopanga kutembelea Zanzibar.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjp8YM4kMiOLnPqJdxsVKYSff5nM0JTQVHfduZdwzvLmvEzj8McNYka7Qpgug64RgSsq8BrXZCbOQ4krW6yOg8--_VtS2yi1J8Ev3UaaCrSjMce1P-AVfg6-ZKj3FBnXed5WghL3RdAWJ869aMkqqGWVIC_vrfaKAunFY3NyTax0Kio8yHjfLj8Qojj6g/s16000/IMG-20221029-WA0057.jpg)
Hivyo amesema kuwa kwa sasa kunahitajika misaada ya hali na mali, sambamba na juhudi za pamoja ili kukabiliana na janga hilo, ambapo kila mmoja anawajibika kusaidia kwamujibu wa uwezo na nafasi yake.
Aidha, Mheshimiwa Othman amesisitiza umuhimu wa kujenga uelewa kwa wananchi na jamii kwa ujumla, juu ya maambukizo hayo kwa kutumia mbinu mbalimbali, zikiwemo njia za sasa za mawasiliano, huku akipongeza juhudi zinazochukuliwa na waganga na wauguzi wa hospitali hiyo, katika kukabiliana na mlipuko wa maradhi ya surua.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVRU2bVo5bgGc-KerQ8N7YBZKn8_PXZRgnflWazbKhlLtraGWhFcAePiBLXqkl8t_V_eDVIHAjVR1o9im4-oZxwTd_pl58GNTWBRIK9IL9LX3FBMtiGfMgjuQ5GKWczR5kaKmYJCFk6thaWAIadcZfaf8b7-ImABcO9J27nj9Rr3LffPgAFvbC77rBFQ/s16000/IMG-20221029-WA0051.jpg)
Akigusia juu ya mtawanyiko wa kuenea kwa maradhi hayo hapa Visiwani, Dokta Slim amezitaja Wilaya za Magharibi A na B Unguja, kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo za kijografia na uwezo wa kipato miongoni mwa wananchi na wakaazi wake, huku akibainisha Mkakati wa Kampeni ya Nyumba kwa Nyumba, kwa ajili ya kuwapatia Chanjo, Watoto chini ya Umri wa Miaka 5, ifikapo Novemba 10, Mwaka huu.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEigjIRyeTYZPTf4BNT9vy1J56jdNCQJdm34ETVjimyhhyCKicekzNh4qb0hH67LGZ97a1MJhPkhTmQjhlSiwvI4mwOV9YHOJEobKyqpuBgW-CTZ-qeDuprXIDWV_6GoCkBgyS07ih0-58Wf4oHl7Zg4PmNbLOus7RNjRGuDwhTxy2ahsq7SfQKqTtluew/s16000/IMG-20221029-WA0052.jpg)
Kwa mujibu wa takwimu za wizara hiyo, takribani watu 1315 wamepata maambukizo ya ugonjwa huo wa surua unaotibika na ambao unaambukizwa na virusi, tangu ulipolipuka hapa Visiwani mnamo Julai mwaka huu; 997 kutoka Unguja, na 318 kisiwani Pemba, huku watoto wapatao nane wakiwa tayari wamefariki.