NA ADELADIUS MAKWEGA
WAKRISTO wameambiwa kuwa kila wanapokwenda kanisani wanaabudu, wanasali,wanasikiliza neno la Mungu na kuomba msamaha ili kupata neema ya Mungu na vile vile wanakwenda kufahamu mambo yanayompendeza Mungu, kumshukuru Mungu kwa yale mema anayotenda katika maisha yetu yao.
Akiendelea kuhubiri Padri Mrema amesema kuwa, kila mara mkristo anapokwenda kusali anahimizwa na masomo ya jumapili hii juu ya toba.
Ameongeza kuwa, si vizuri kujiona wewe ni mwenye haki zaidi ya mwingine, mbele ya Mungu tuyaone madhaifu yetu na kujinyenyekeza.
Misa hiyo pia ilikuwa na maombi kadhaa likiwamo ombi hili,“Eee Baba Mungu sisi ni kama mtoza ushuru, hatuna kitu mbele yako, usikilize sala zetu katika unyenyekevu tunaokutolea kila siku.”