NA MATHIAS CANAL-WEST
SERIKALI kupitia Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) ina mpango wa kuanzisha Kampasi ya MUHAS mkoani Kigoma.

Aidha,kampasi hiyo inatarajiwa kuwa na miundombinu itakayotoa mazingira bora ya ufundishaji na kujifunzia, utafiti pamoja na utoaji wa huduma kwa jamii.

Waziri Mkenda amesema kuwa, serikali kupitia mkopo wa Benki ya Dunia imetenga kiasi cha dola za Marekani milioni 45.5 kwa ajili ya MUHAS.
Kati ya fedha hizo, amesema kiasi cha dola za Marekani milioni 15 zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu katika kampasi ya Kigoma.

Prof.Mkenda amesema kuwa,ujenzi huo umefadhiliwa na Serikali ya Canada kupitia Mradi wa Kuendeleza Elimu ya Ualimu nchini (Teachers Education Supports Project-TESP).
Mradi wa ujenzi wa Chuo cha Ualimu Kabanga ulianza tarehe 26/03/2019 na ulikamilika tarehe 22/04/2022.
Ujenzi umetekelezwa na Mkandarasi SUMA JKT Kanda ya Magharibi chini ya Usimamizi wa Mshauri Elekezi Bureau for Industrial Cooperation (BICO) wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Aidha, kazi ya utengenezaji na uwekaji wa Samani katika majengo haya inaendelea.