NA FRESHA KINASA
KATIKA kuadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia, Shirika la Hope for Girls and Women in Tanzania (HGWT) kwa kushirikiana na Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Serengeti mkoani Mara wametoa elimu ya ukatili wa kijinsia katika Shule ya Msingi Mapinduzi Day iliyopo wilayani Serengeti na msaada wa taulo kwa wanafunzi wa kike shuleni hapo.
Kauli mbiu ya mwaka huu inasema 'kila uhai unathamani tokomeza mauaji na ukatili wa wanawake na watoto' ambapo yamaenza rasmi Novemba 25, 2022 na kilele chake itakuwa Desemba 10, 2022.

Ambapo lin avituo viwili kikiwemo Kituo cha Nyumba Salama Kiabakari kilichopo wilayani Butima na Kituo cha Hope Mugumu Nyumba Salama katika Wilaya ya Serengeti.
Vituo hivyo hutoa hifadhi kwa wasichana ambao hukimbia ukatili wa aina mbalimbali ikiwemo ukeketaji na ndoa za utotoni pamoja na kuwapa msaada wa kisaikolojia, mahitaji yao muhimu, kuwaendeleza kielimu na kifani wakiwa katika vituo hivyo ili wafikie ndoto zao.

"Mfano ukeketaji una madhara ikiwemo kutoka damu nyingi wakati wa kukeketwa, kuandaliwa kuozeshwa na hivyo kukatisha masomo, hatari ya kupata magonjwa ya kuambukiza, kuathiri kisaikolojia kutokana na kufanyiwa ukeketaji kwa lazima pamoja na kupata ulemavu kwa hiyo ukeketaji haufai lazima upingwe."amesema Goodluck.

Pia, amewaomba wanafunzi hao kuwa mabalozi wa kutoa elimu ya madhara ya ukatili wa kijinsia waliyoipata katika kuhakikisha kwamba ukatili unakwisha.
Suzan John ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya Sekondari Twiboke ambaye anaishi Kituo cha Hope Mugumu Nyumba Salama baada ya kukimbia ukeketaji kutoka kwao, ameiomba serikali kuendelea kutoa elimu kwa jamii na kusimamia vikali sheria kuwaadhibu wanaofanya vitendo vya ukatili kwani wanakwamisha watoto wa kike kufikia ndoto zao.
Kwa upande wao wanafunzi wa kike shuleni hapo wakizungumza na DIRAMAKINI wamepongeza kutolewa kwa elimu hiyo sambamba na kupewa taulo za kike, kwani zitawasaidia kujistiri na kuondokana na kutohudhuria masomo wakati wa hedhi.

Pi, amepongeza kazi zinazofanywa na Shirika la Hope for Girls katika kupambana na vitendo vya ukatili na kuwasaidia wasichana kufanikisha malengo yao kwa kuwapa mahitaji muhimu na kuwaendeleza kielimu.

Amesema, Dawati la Jinsia na Watoto Wilaya ya Serengeti limejipanga kwa kushirikiana na Shirika la Hope for Girls and Women in Tanzania na wadau mbalimbali kuunda mabaraza katika shule za msingi na sekondari wilayani humo.

Tags
Habari
HGWT
Kataa Ukatili
Mkoa wa Mara
Serengeti
Siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijinsia
Unyanyasaji na Ukatili wa Kijinsia