Ndugu Abdulrahman Omari Kinana, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Bara;
Ndugu Daniel Godfrey Chongolo, Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi;
Ndugu Dkt. Philip Isdor Mpango, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Ndugu Hemed Suleiman Abdulla, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar;
Ndugu Christina Solomon Mndeme, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Bara;
Ndugu Dkt. Abdallah Juma Saadala, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar;
Ndugu Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa;
Ndugu Viongozi Wastaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar;
Ndugu zetu Wenza wa Viongozi mliopo hapa;
Ndugu Wajumbe kutoka Vyama vya Siasa Rafiki; na
Waheshimiwa Mabalozi kutoka nchi mbalimbali mliopo hapa;
Wasilisho hili ni muhtasari wa taarifa ya kina iliyopo katika vitabu viwili vikubwa ambavyo kila mmoja wetu amepatiwa.
Chini ya uongozi wako mahiri na kuhimiza ulipaji kodi kwa hiari, ukusanyaji wa mapato ya Serikali umeendelea kuongezeka hadi kufikia wastani wa shilingi trilioni 1.74 kwa mwezi ikilinganishwa na shilingi trilioni 1.46 kwa mwezi mwaka 2020/2021.
Tarehe 4 Aprili, 2022 hapa hapa mkoani Dodoma, ulikabidhi vitendea kazi kwa maafisa ugani wote nchini zikiwemo pikipiki 2,000, vifaa vya kupima afya ya udongo 143, simujanja 384 na visanduku vya ufundi 3,400 vya maafisa ugani.
Kutokana na juhudi zako, baadhi ya Marais na Wakuu wa Nchi waliotembelea Tanzania ni Waheshimiwa Yoweri Museveni (Uganda), Felix Tshisekedi (Jamhuri Kidemokrasia ya Congo), Filippe Nyusi (Msumbiji), Evariste Ndayishimye (Burundi), Hakainde Hichilema (Zambia) na William Ruto (Kenya).
Kipindi cha Novemba, 2020 hadi Oktoba, 2022 Serikali imejenga mtandao wa barabara kwa kiwango cha lami wenye urefu wa kilomita 950.29.
Hadi Oktoba 2022, ujenzi wa gati 1-7 katika Bandari ya Dar es Salaam unaohusisha kuongeza kina, kujenga Gati Maalumu (RoRo berth) ya kuhudumia meli za magari na kujenga yadi ya kuhudumia makasha (container yard) umekamilika.
Pia, limerudisha safari za kikanda katika vituo vya Bujumbura, Entebbe, Harare, Lusaka na Hahaya pamoja na kuanzisha vituo vipya vitatu katika miji ya Lubumbashi, Nairobi na Ndola.
Na hadi kufikia Septemba 2022, takwimu zinaonesha kuwa watalii wanaokuja nchini Tanzania wameongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 na kufikia 1,034,180.
Vivutio vya utalii tulivyonavyo vimeifanya sekta hii kuwa mhimili muhimu wa uchumi na sasa Tanzania imeanza kuwa kitovu cha utalii wa mikutano (conference tourism) ambapo hivi karibuni tumeweza kuwa wenyeji wa Mkutano wa 65 wa Shirika la Utalii Duniani - Kamisheni ya Afrika.
Zoezi la kuandikisha wakazi wanaoomba kuhama kwa hiari linaendelea vizuri. Aidha, hadi kufikia tarehe 20 Oktoba, 2022 jumla ya kaya 1,524 zenye watu 8,715 na mifugo 32,842 zilikuwa zimekwishajiandikisha.
Aidha, kati ya tarehe 16 Juni, 2022 na tarehe 15 Novemba, 2022 makundi 16 yenye kaya 489 zenye watu 2,629 na mifugo 14,132 zilikuwa zimeshahamia katika kijiji cha Msomera, wilayani Handeni.
Miji mingine ni Chamwino, Mugumu, Kasulu, Mpanda, Sikonge, Urambo, Kaliua, Kayanga, Geita, Chato, Mafinga pamoja na ukanda wa Makonde. Utekelezaji wa miradi hiyo ni mojawapo ya mikakati ya Serikali ya kusambaza maji safi na salama maeneo ya mijini na vijijini.
Aidha, shilingi bilioni 136.51 zilitolewa kununua vifaa na vifaa tiba ambavyo vinaendelea kusambazwa maeneo mbalimbali nchini.
Fedha hizi zimetumika kujenga vyumba vya madarasa 12,000 katika shule za sekondari, vyumba vya madarasa 3,000 katika vituo shikizi na mabweni 50 kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Utekelezaji wa mpango huo umepunguza uhaba wa miundombinu ya shule katika shule za msingi na sekondari.
Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 104.2 zimepangwa kutekeleza miradi 218; shilingi bilioni 17.5 kununua seti 25 za mitambo ya kuchimba visima; shilingi bilioni 17.6 kununua seti 5 za mitambo ya ujenzi wa mabwawa pamoja na seti 4 vifaa vya utafiti wa maji.
Pia imefungua Konseli Kuu mbili ikiwemo jiji la Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na jiji la Guangzhou, China na kuratibu mikutano 25 ya ubia wa maendeleo baina ya Tanzania na nchi za Afrika, Ulaya, Amerika, Asia, Australasia na Mashariki ya Kati.
Vilevile, lugha ya Kiswahili imetambulika na kuidhinishwa kama lugha rasmi katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Jumuiya ya Maendeleo Kusini Mwa Afrika na Umoja wa Afrika na tarehe 7 Julai ya kila mwaka imetangazwa kuwa Siku ya Kiswahili Duniani.
Katika kipindi cha Novemba 2020 hadi Desemba 2022, Serikali iliratibu vikao vitatu vya Kamati ya Pamoja ya SMT na SMZ na vikao 30 vya ushirikiano baina ya sekta zisizo za Muungano za SMT na SMZ.