NA MWANDISHI WETU
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango amesema, kuna baadhi ya viongozi kwa maslahi yao binafsi wanachangia katika uharibifu wa mazingira.

"Wapo baadhi ya viongozi kwa maslahi binafsi, wanachangia sana kwenye uharibifu wa mazingira.

Katika kongamano hilo amesema, mwaka 1980 uharibifu wa mazingira ulifanywa kwa asilimia 42; mwaka 1980 asilimia 50 na mwaka 2012 uharibifu ulikuwa kwa asilimia 68.

"Sisi tunafanya habari za uchunguzi na tumebaini Ranchi ya Usangu inamilikiwa na familia 12, wamo majaji, wamo wabunge, wamo mawaziri na leo nitakukabidhi majina.
"Ranchi hii ilifutwa na GN No. 28 lakini kamati ya mawaziri wanane iliamua kuiacha," amesema Balile.

"Leo Mto Ruaha Mkuu umefikisha siku 130 bila kutiririsha maji, na ukienda hifadhini utasikitika kuona viboko wanagombania mchanga na si maji kutokana na uharibifu wa mazingira,"amesema Mchange.