NA JONH MAPEPELE
WANANCHI wa eneo la Nyanda na Utunge wilayani Rufiji wamemshukuru Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mbunge wa Rufiji na MNEC wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Mohamed Mchengerwa kwa kutatua mgogoro wa muda mrefu baina ya mwekezaji wa mradi wa uzalishaji wa sukari na wananchi wa maeneo hayo.

Amesema mgogoro huo baina ya mwekezaji huyo ambaye ni Lake Agro unatokana na ukiukwaji wa makubaliano ya awali ya kupewa eneo la uwekezaji na kutopata taarifa sahihi za uwekezaji.