NA MWANDISHI WETU
NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete ameitaka Bodi ya Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) kuhakikisha miradi yote inayotekelezwa na kampuni hiyo inakamilika kwa wakati na kuzingatia thamani ya fedha.
Naibu Waziri wa Uchukuzi Atupele Mwakibete (kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni za Huduma za Meli Tanzania (MSCL) Erick Hamisi, wakati wa zoezi la ushushwaji wa meli ya Mv. Mwanza katika Ziwa Victoria, jijini Mwanza.
Naibu Waziri Mwakibete ametoa kauli hiyo jijini Mwanza wakati wa hafla ya ushushaji wa meli ya MV Mwanza hapa kazi tu ambayo ujenzi wake kwa sasa umefikia asilimia 82.


Muonekano wa Meli mpya ya Mv Mwanza “Hapa kazi tu” inayojengwa na kampuni za Gas Enter Ship-Building Engineering na Lang Nam Corporation za nchini Korea, baada ya kushushwa katika Ziwa Viktoria jijini Mwanza.

.jpg)


