NA MWANDISHI WETU
SERIKALI ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Samia Suluhu Hassan umeweka historia kubwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo.
Mkuu wa Idara ya Kitendo cha Mionzi na Picha katika Hospitali hiyo , Dkt.Goodluck Mbwilo amesema kwamba wanaishukuru Serikali kwa uwekezaji huo mkubwa ambao umeandika historia kwa mkoa huo ambapo awali hawakuwahi kuwa na mashine kama hiyo kutokana na kwamba mashine hizo zilikuwa zikipatikana kwenye hospitali za Rufaa za Kanda na Taifa.
Amesema, kwenye hospitali hizo ndio zilikuwa zikipatikana lakini kwa sasa kila hospitali ya mkoa kupitia Rais Dkt Samia ameweza kufanikisha hilo na hiyo itasaidia kutoa huduma bora kwa watanzania wakiwemo wagonjwa wa ajali na wenye matatizo ambao wanahitaji huduma ya CT Scan kwa ajili ya uchunguzi.
“Kwa kweli tunaishukuru Serikali ya awamu yaa Sita kwa uwekezaji huu mkubwa ambao awali haukuwepo haya ni mapinduzi makubwa kwenye sekta ya afya kwa mkoa wetu hivyo niwaombe wananchi watumie fursa hiyo kujitokeza kuweza kuja kupata vipimo,”amesema.
Hata hivyo, amesema kwa sababu gharama za vipimo zipo chini ukilinganisha na hospitali binafasi huku akiwashauri watanzania hususani wakazi wa Mkoa wa Tanga na mikoa mengine kuchangamkia mpango wa fursa ya kuwa na bima ya afya ili kuwarahisishia kupata huduma za matibabu pindi wanapokuwa wakiugua.