NA CATHERINE SUNGURA
MGONJWA mmoja wa Marburg mwenye umri wa miaka 26 ameruhusiwa akiwa na afya njema na jamii imetakiwa kumpokea vyema na kushirikiana nae katika shughuli zake.

“Ninayo furaha kubwa kuwajulisha kuwa leo tumemruhusu mgonjwa mmoja mwanaume mwenye umri wa miaka 26 akiwa na afya njema, ni matumaini yangu jamii itampokea vyema na kushirikiana nae kama kawaida, ni jambo la kumshukuru Mungu kuwa hatujapata wagonjwa wapya wala vifo.”

Hata hivyo Waziri amesema kuwa jumla ya watu 212 waliotengamana na wagonjwa wamebainishwa na kati ya hao watu 35 wamemaliza siku 21 za uangalizi bila kuonesha dalili zozote za ugonjwa .
“Hii ni ishara nzuri sana kwetu, Wizara ya afya , serikali na taifa kwa ujumla kwa kuwa maambukizi ya Virus vya Marburg nchini yamedhibitiwa kwa wakati.Serikali bado inahimiza wananchi wote na hasa wa Mkoa wa kagera kuendelea kuchukua tahadhari, kudhibiti na kuzuia maamb ukizi mapya katika jamii”.
