NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Utamaduni, Sana na Michezo , Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana amesema, wizara inakaribisha wadau kushiriki katika shughuli za Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwemo matamasha, ligi za michezo mbalimbali katika ngazi zote.

Wadau hao ni Bw.Japhet Mswaki ambaye ni Mratibu wa Tamasha la Yakwetu Fair Festival, Bw. Rukemo Maasai Muaandaaji wa Tamasha la Maasai Festival pamoja na Bw.Fatih Karakus anayejihusisha na uibuaji wa vipaji vya michezo.
Aidha,Mhe. Balozi Pindi Chana amekutana na Waandaaji wa Tamasha la Pasaka mwaka huu wakiongozwa na Muimbaji wa nyimbo za injili, Christina Shusho ambalo amesema linalenga kuendelea kuhamasisha jamii kushirikiana na kukumbushana upendo, mila na desturi za Kitanzania pamoja na kutoa burudani.