Awamu ya Pili, Safisha Pendezesha Dar es Salaam yatangazwa

NA DIRAMAKINI

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, CPA Amos Makalla ametangaza kuanza kwa awamu ya pili ya kampeni ya SAFISHA PENDEZESHA DAR ES SALAAM baada ya awamu ya kwanza ya kampeni hiyo iliyodumu kwa mwaka mmoja na miezi mitano kuwa na mafanikio makubwa ikiwemo kufanya Jiji hilo kushika nafasi ya sita kwa usafi Afrika. 
Akizungumza wakati wa kikao kazi cha tathimini awamu ya kwanza na kuweka mikakati ya awamu ya pili,CPA Makalla ameelekeza watendaji kuanzia ngazi ya mkoa, wilaya,kata na mitaa kusimamia ufanyaji usafi. 

Aidha, CPA Makalla amesema miongoni mwa mambo yayopaswa kuwekewa mkazo zaidi ni udhibiti wa ufanyaji biashara holela, usafishaji mazingira, upendezeshaji na upandaji miti kwenye bustani. 

Kutokana na mwamko mkubwa wa usafi uliopo, RC Makalla ameelekeza kila halmashauri kushirikiana na wadau ambao wapo tayari kupendezesha Jiji huku akielekeza taasisi za TANROADS, TARURA na DAWASA kufanya kazi kwa ushirikiano. 
Pamoja na hayo, CPA Makalla amesema lengo la kampeni hiyo ni kufanya Dar es Salaam izidi kushika nafasi za juu kwa usafi Afrika jambo litakalosaidia kudhibiti pia mlipuko wa magonjwa ya mlipuko ikiwemo Kipindupindu na hata kudhibiti maambukizi ya malaria. 

Hata hivyo, RC Makalla ameendelea kusisitiza Wananchi kufanya usafi Kila ifikapo jumamos ya mwisho wa Mwezi huku akiwataka wafanyabiashara kufanya biashara kwenye maeneo waliyopangwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news