NA MWANDISHI WETU
MAMLAKA ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) wameazimia kuboresha na kukarabati miundombinu ya ndani na nje ya Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K Nyerere uliopo barabara ya Kilwa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke jijini Dar es salaam.


"Lengo ni kuendelea kuboresha miundombinu ya maonesho ili kuweka mazingira mazuri ya uoneshaji wa bidhaa kwa wafanyabiashara pamoja na watembeleaji na kuleta matokeo yenye tija," alisema.