DODOMA-Anaandika Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan, "Leo nchi yetu inaadhimisha siku adhimu kuwakumbuka mashujaa wetu.

Tunajenga mnara mrefu zaidi barani Afrika katika Jiji la Dodoma kama sehemu ya kuendelea kuwaenzi mashujaa wetu.

Nawaelekeza Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Fedha na wote wanaohusika na ujenzi huu wa kihistoria kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kwa viwango.


Mwenyezi Mungu Ibariki Afrika.
Mwenyezi Mungu Ibariki Tanzania.