NA FRESHA KINASA
HALMASHAURI ya Wilaya ya Musoma kwa kushirikiana na Shirika lisilo la kiserikali la Victoria Farming and Fishing Organization (VIFAFIO) lililopo Musoma mkoani Mara wamezindua Mwongozo wa Taifa wa Dawati la Ulinzi na Usalama wa Mtoto ndani na nje ya shule katika shule za sekondari mbili na shule za msingi tatu zilizopo katika halmashauri hiyo.

Uzinduzi huo umefanyika Julai 26, 2023 katika shule hizo kwa kuzingatia muundo wake wakiwemo walimu wawili wa malezi na unasihi upande wa Mtiro Sekondari na Nyanja Sekondari ambao wataratibu na kusimamia dawati hilo na wajumbe ambao ni wanafunzi 11 ambao wamechaguliwa kwa kuzingatia jinsi na mjumbe mmoja kutoka bodi ya shule.
Huku upande wa shule ya msingi Majita 'A', Nyabaengere na Msanja shule ya Msingi wakichaguliwa wanafunzi 15 kwa kila shule kwa mujibu wa mwongozo huo, walimu walezi wawili na unasihi, wanafunzi wenye ulemavu wawili, pamoja na mwakilishi mmoja kutoka kamati ya shule ya msingi ambao watajumuika kuunda dawati hilo.

Aidha, Wangaso ameongeza kuwa, kupitia dawati hilo manufaa makubwa yatapatika ambayo yatasaidia kwa kiwango kikubwa kuweza kuimarisha mapambano ya vitendo vya ukatili wa kijinsia.


Erasto Peter ambaye ni mwanafunzi wa Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Nyanja amesema kwamba, kupitia mwongozo huo atajifunza mambo mengi yatakayomsaidia kutoa elimu kwa wenzake juu ya madhara ya vitendo vya ukatili na sehemu sahihi za kuripoti matukio ya ukatili.

"Tunataka kutokomeza aina zote za ukatili wa Kijinsia katika Jamii yetu upo ukatili wa Kimwili, wa kingono, kisaikolojia, kiuchumi na mara nyingi wenye uwezo wamekuwa wakiwafanyia ukatili wasio na uwezo hii ni mbaya sana. Na mara nyingi wanaofanyiwa ukatili pia na wao huwa wanakuja kuwa watendaji wakubwa wa ukatili kwa wenzao,"amesema Gichaine.

Gichaine ameishauri jamii kuachana na vitendo vya ukatili wa kijinsia, kwani vinarudisha nyuma maendeleo na kwamba ukatili ni kinyume cha sheria na haki za binadamu na una madhara mengi ikiwemo ulemavu na kuathiri afya ya kisaikolojia na magonjwa ya kuambukiza hasa vitendo vya ubakaji.