DODOMA-Serikali kupitia Wizara ya Afya inaendelea kushirikiana na wadau wa huduma za uchunguzi wa magonjwa kwa kuimarisha huduma za uchunguzi wa maabara, Vifaa-Tiba, damu salama pamoja na ubora wa huduma ili kutekeleza maelekezo ya Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu.

“Tunaendelea kushirikiana na wadau hawa ili kuondoa kero kwa wananchi ambapo miongoni mwa kero hizo ni pamoja na upatikanaji wa Vitendanishi, Vifaa, Vifaa-Tiba ikiwemo ya mionzi na upande wa damu salama,”amesema Dkt. Magesa.

“Lengo la mkutano huo ni kuwasiliana na kujadili vipaumbele vya huduma za uchunguzi wa magonjwa kwa wadau wote ili kuweka mikakati ya pamoja ya kufikia malengo ya Wizara ya Afya katika kuimarisha huduma za uchunguzi wa magonjwa,”amesema Dkt.Magesa.

“Katika kutekeleza malengo aliyoyatoa Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu ndio maana tumeamua kukutana ili tuweze kujadiliana namna ya kutekeleza maelekezo hayo ili tuweze kuwahudumia wananchi kwa urahisi na haraka,”amesema Dkt. Magesa.

“Lakini pia mashirikiano haya yatawezesha kupatikana kwa wakati takwimu sahihi ili kuhakikisha tunaleta huduma za uchunguzi wa haraka kwa wananchi na wananchi wafurahiye matunda ya uwekezaji kwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan lakini pia na Waziri wetu Mhe. Ummy Mwalimu (MB),”amesema Dkt. Magesa.
