ARUSHA-Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amesema, mikutano ya Kimataifa inayofanyika hapa nchini ni fursa ya kutangaza lugha adhimu ya Kiswahili ambayo ni mojawapo ya Lugha Rasmi ya Kikazi ya Umoja wa Afrika (AU) pamoja na Jumuiya kadhaa za Kikanda barani Afrika.

Mhe. Ndumbaro ameongeza kuwa, Tanzania ina wataalamu katika tafsiri na ukalimani, hivyo wana uwezo wa kutoa huduma ya ukalimani katika mikutano hiyo.
Kikao hicho kimeongozwa na Mhe.Balozi Dkt.Pindi Chana,Waziri wa Katiba na Sheria na kuhudhuriwa na Mhe.Haroun Suleimani,Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi na Utawala Bora wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Tags
Baraza la Kiswahili la Taifa
Habari
Kiswahili Afrika Mashariki
Michezo
Siku ya Kiswahili Duniani