NA VERONICA SIMBA
REA NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt Dotto Biteko amesema serikali imetoa shilingi bilioni 170 kwa ajili ya utelekezaji wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) mkoani Mtwara.

Naibu Waziri Mkuu ameipongeza REA kwa usimamizi mzuri wa miradi ya usambaji wa nishati vijijini ili kuhakikisha utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya upatikanaji wa nishati vijijini ifikapo 2025 inatimia.
Aidha, Dkt Biteko ameitaka REA na TANESCO kutumia vifaa vya usambazaji umeme vinavyozalishwa na viwanda vya ndani badala ya kuagiza nje ya nchi .

Amesema katika kukuza viwanda vya ndani, REA na Tanesco wanapaswa kuhakikisha inatumia bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani kuchochea ukuaji wa uchumi na upatikanaji wa ajira kwa wananchi.

Amesema wafanye tathimini ya wakandarasi na kuahidi kurudi baada ya miezi mitatu kuhakikisha wamekamilisha kama alivyoagiza.


