MOROGORO-Wito umetolewa kwa wananchi kuendelea kujitokeza kupima VVU kwa hiari ili kujua hali zao ili kuendelea kuishi kwa kuzingatia matokeo, kwa wale ambao hawatakutwa na maambukizi ni nafasi kwao kuendelea kuishi ili wasiambukizwe na wale ambao watakutwa na maambukizi wana nafasi kuendelea kuishi kwa kutumia dawa za kufubaza.
Ameongeza kusema tafiti zote za miaka mitano zimeonesha wanaume hawajitokezi kupima, na hawajitokezi kuanza kupata dawa, na hivyo kusumbuliwa sana na magonjwa Nyemelezi yanayotokana na virusi vya UKIMWI.
“Virusi vya UKIMWI na UKIMWI upo ni wajibu wa kila Mwananchi kuendelea kuchukua tahadhari,” alibainisha
Akizungumzia kuhusu malezi, ametoa rai kwa wazazi kukaa na familia na kuwaelimisha uwepo wa tatizo hili la UKIMWI.
“Tunajukumu kubwa la kuendelea kutoa malezi bora kwa watoto wetu na kuwajengea misingi ya tabia njema,” alifafanua.

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Adam Malima akiongea jambo wakati wakikao cha maandalizi kuelekea siku ya UKIMWI kitaifa.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe.Adam Malima amesema, maandalizi kuelekea wiki Maadhimisho ya siku ya UKIMWI yanaendelea vizuri