THE HAGUE-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Yusuf Makamba (Mb.) amewasili Jijini The Hague, Uholanzi kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 13 hadi 15 Novemba 2023.

Aidha, pembezoni mwa kongamano hilo, Mhe. Waziri Makamba atapata nafasi ya kukutana na Waziri mwenzake wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Mhe. Kanke Bruins Slot. Kadhalika, Mhe. Makamba anatarajiwa pia kukutana na kufanya mazungumzo na Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Uholanzi (Tanzania Diaspora).




