DAR ES SALAAM-Ofisi ya Msajili wa Hazina imeng’ara kwa kuibuka mshindi wa kwanza katika tuzo za uandaaji wa taarifa za fedha kwa mwaka 2023 katika kundi la Idara Huru za Serikali (Independent Government Department).
Tuzo hizo zimetolewa mwishoni mwa wiki na Bodi ya Taifa ya uhasibu na ukaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Ofisi ya Msajili wa Hazina iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Usimamizi, wa Utendaji, Ufuatiliaji na Tathmini – Mashirika ya Kibiashara, Bi. Lightness Mauki akiambatana na Mkurugenzi wa Fedha na Uhasibu wa Taasisi hiyo Hassan Mohamed, kwa niaba ya Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu.
Akizungumza mara baada ya kupokea tuzo hiyo, Bi. Mauki amesema kuwa ushindi walioupata utaongeza chachu ya kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuimarisha utendaji kazi katika taasisi yao.
Bodi ya Taifa ya uhasibu na ukaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imekuwa na utaratibu wa kila mwaka kutoa tuzo kwa Mashirika na Taasisi za Serikali zilizofanya vizuri kutambua kazi wanazofanya.