DCEA yashiriki mafunzo usimamizi salama wa kemikali Kanda ya Kati

DODOMA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Kati imeshiriki katika mafunzo ya usimamizi salama wa kemikali kwa wadau wa kemikali wa kanda hiyo yaliyoandaliwa na Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Kati.
Katika mafunzo hayo, Kamishna Msaidizi wa Sayansi Jinai wa DCEA, Ziliwa Machibya, amewasilisha mada kuhusu kemikali bashirifu na madhara ya uchepushaji wa kemikali hizo.
Akizungumzia mafunzo hayo, Kaimu Kamishna Msaidizi wa Kanda, Dkt. Christian Mbwasi, amesema, mamlaka itaendelea kushirikiana kikamilifu na Ofisi ya Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali pamoja na wadau wa kemikali katika kuhakikisha wanasimamia kwa usahihi na kuzuia uchepushwaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news