DCEA yatoa elimu ya dawa za kulevya kwa wafanyakazi wa bandari

MWANZA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini (DCEA) imeendesha mafunzo na kutoa elimu kwa watumishi wa Bandari ya Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla kuhusu dawa za kulevya.
Dezdel Tumbu ambaye ni Afisa Elimu wa DCEA Kanda ya Ziwa amesema, wanafanya hivyo kwa sababu bandari ni sehemu ambazo wauzaji na wasafirishaji wa dawa za kulevya huwa wanapatumia mara nyingi.

"Wauzaji na wasafirishaji wa dawa za kulevya wanaingiza mizigo na kutoa mizigo yao kupitia bandari.

"Kwa hiyo tunaamini kabisa kwamba kwa kuwaelimisha na kuwajengea uwezo maofisa wa bandari watatusaidia katika kufanya ukaguzi.

"Lakini pia kutambua mizigo ambayo inaweza kuingia ambayo inahusishwa na dawa za kulevya ili tatizo hili la biashara ya dawa za kulevya na matumizi liweze kuisha,"amesema Tumbu;

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news