
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende, akiwasili kwenye viwanja vya Nyerere Square alipotembelea mabanda ya wadau mbalimbali wanaoshiriki Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea Jijini Dodoma kwa lengo la kuona namna wadau hao wanavyotekeleza majukumu yao ya kila siku.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akisaini vitabu vya Taasisi zinazoshiriki Maadhimisho ya Wiki ya Sheria mara baada ya kutembelea Mabanda ya Taasisi hizo kwa lengo la kuona namna taasisi hizo zinavyotekeleza majumu yao ya kila siku.





Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akimsikiliza Wakili wa Serikali wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Bi. Neema Taji alipotembelea Banda la Ofisi hiyo wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayoendelea jijini Dodoma.
