OSLO-Tanzania na Norway zimetia saini hati ya makubaliano (Memorandum of Understanding- MOU) ya Ushirikiano wa Kilimo na Usalama wa Chakula tarehe 14 Februari, 2024 katika ukumbi wa Climate House (Garden Avenue) Oslo nchini Norway.

Makubaliano hayo yamelenga kuimarisha masuala ya utafiti, biashara ya mazao ya kilimo, kuimarisha vyama vya ushirika na kilimo himilivu kwa mabadiliko ya tabianchi.