MBABANE-Mheshimiwa Balozi Phaustine Kasike amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu wa Ufalme wa Eswatini, Mhe. Thulisile Dladla.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Machi 30,2024 na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Maputo,Msumbiji.


Kwa upande wake, Mhe. Balozi Kasike aliishukuru Serikali ya Ufalme wa Eswatini kwa ushirikiano aliopata wakati wote akiwa nchini Eswatini na kusisitiza umuhimu wa kutekelezwa masuala yote yaliyokubalika wakati wa ziara hiyo kwa maslahi ya Serikali na wananchi wa Tanzania na Eswatini.