ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema, misikiti inatakiwa kutumika kutatua changamoto zilizopo katika jamii.

Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amewahimiza Waumini wa Dini ya Kiislamu kuitumia Misikiti kufanya ibada kwa wingi hususani kuelekea kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
Kwa upande mwingine Rais Dkt.Mwinyi amesema kuna wajibu wa kuwafundisha watoto elimu ya dini mapema.

Rais Dkt.Mwinyi ametoa shukrani kwa wafadhili waliofanikisha ujenzi wa msikiti huo.