NA GODFREY NNKO
SERIKALI kupitia Wizara ya Madini inatarajia kutumia shilingi bilioni 35 kujenga jengo pacha la Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha, ambalo litasaidia kuongeza udahili kutoka wanafunzi 180 hadi 450 kwa mwaka.

Mhandisi Maganga amesema, jengo hilo litakuwa na miundombinu mbalimbali ikiwemo madarasa, makumbusho, masoko ya madini ya vito, karakana za uongezaji thamani madini, maabara za madini ya vito na bidhaa za usonara, ofisi na mabweni ya wanafunzi.
Amesema, jengo hilo litakuwa mahsusi kwa utoaji wa mafunzo ya kuongeza thamani madini ya vito,minada ya madini ya vito na maonesho ya madini.
Mhandisi Maganga ameongeza kuwa, jengo litatimiza ndoto kubwa ya Serikali ya Tanzania kwa kulifanya eneo hili kuwa kitovu cha madini ya vito barani Afrika, hii ni kutokana na wingi wa rasilimali madini ya vito yaliyopo nchini.

Akielezea kuhusu hali ya teknolojia ya uthaminishaji, Mhandisi Maganga amesema kuwa,bado nchi za Afrika zina changamoto kubwa ya teknolojia ya kusanifu madini, hivyo TGC itakuwa mkombozi mkubwa kwa wadau mbalimbali wa madini ya vito na metali hususani katika kuchakata na uthaminishaji.
Mradi huu unatarajia kukamilika ndani ya miaka miwili ijayo baada ya taratibu zingine kukamilika.
This comment has been removed by a blog administrator.
ReplyDelete