KAGERA-Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mheshimiwa Fatma Mwassa amewataka maafisa tarafa na watendaji wa kata kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani na matumizi yake kwa kuwa Serikali inaendelea kusisitiza matumizi ya mifumo ya kielektroniki katika ukusanyaji wa mapato.
Ameyasema hayo Aprili 23, 2024 wakati wa akifunga mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa tarafa na watendaji wa kata wa Mkoa wa Kagera yaliyofanyika kwa siku mbili katika Ukumbi wa Bukoba Sekondari.

Pia,kuwataka kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato na matumizi yake kwa kushirikiana na viongozi wa wananchi na watendaji wengine walipo katika maeneo yao ya kazi waliopo ngazi ya msingi."Bila ushirikiano hakuna mafanikio," Mheshimiwa Mwassa amesema.

“Nyie ndio mpo katika kazi za msingi mnapaswa kufahamu na kuzingatia kanuni na maadili na kutumia misingi ya haki badala ya upendeleo pale mnapotoa huduma kwa wananchi na kuweka vizuri malengo halisi ya kazi zenu ili kuwawezesha kufikia kiwango cha juu katika utendaji wenu wa kazi kwa kuwatendea haki wananchi katika utoaji wa huduma,”amesema Mheshimiwa Mwassa.