Sasa ni Tume Huru ya Uchaguzi (INEC)

DODOMA- Serikali imesema Tume ya Uchaguzi (NEC) itabadilishwa jina ifikapo Aprili 12, 2024 na itaanza kutambulika kama Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, hii ni kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi.
Taarifa ya Matinyi imesema hatua hiyo inafuatia tangazo la Serikali namba 225 la Machi 29, 2024 la Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi namba 2 ya mwaka 2024, inayoanza kutumika rasmi Aprili 12, 2024.

“Hivyo, kuanzia Aprili 12, 2024 jina la Tume litabadilika na litakuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi au kwa kiingereza ‘Independent National Electoral Commission.”

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news