DAR ES SALAAM-Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) amekutana na Waziri wa Ushirikiano wa Maendeleo na Mabadiliko ya Tabianchi wa Denmark, Mhe. Dan Jørgensen ambapo nchi hizi mbili zimeangazia maeneo ya ushirikiano na kukubaliana kuongeza ushirikiano kwenye sekta za kimaendeleo.
