Waziri Ulega ahimiza Uwekezaji wa mitaji sekta za mifugo na uvuvi

DAR-Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema, sekta za mifugo na uvuvi zinaweza kuwa na tija kubwa zaidi kama taasisi za kifedha zitaendelea kuwekeza mitaji katika shughuli za mifugo na uvuvi ili ziweze kuzalisha kwa tija na hivyo kuchangia vyema kwenye pato la taifa.
Ulega amesema hayo wakati akifafanua baadhi ya hoja za wadau wa Kongamano la Uwekezaji la CRDB lililopewa jina la “Uwekezaji Day 2024”linalofanyika jijini Dar es Salaam leo Aprili 28,2024.

Amesema sekta za mifugo na uvuvi zinaweza kuwa na tija kubwa katika uchumi wa taifa hivy
ni muhimu taasisi za kifedha ikiwemo CRDB kuendelea kuwekeza mitaji ili kuinua wadau wanaojishughulisha na sekta hizo.
“Nawapongeza CRDB kwa kuaandaa Kongamano hili kubwa la uwekezaji day, ombi langu kwenu, jukwaa hili liwe chachu ya kubadili sekta hizi za uzalishaji kwa kuongeza mitaji ili kuchechemua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news