Balozi wa Marekani nchini atembelea Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt.Salim Ahmed Salim

DAR- Mei 23, 2024 Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Michael Battle ametembelea Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt.Salim Ahmed Salim (CFR) jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania,Mhe. Michael Battle (aliyekaa katikati), katika picha ya pamoja na Dkt. Felix Wandwe, ndc Kaimu Mkurugenzi (CFR), (wa pili kulia) baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti na Wawakilishi wa Wanafunzi wakati wa ziara ya Mhe. Balozi Battle ya kutembelea Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim, tarehe 23 Mei, 2024.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Michael Battle ( kushoto) akiwa katika mazungumzo na Dkt. Felix Wandwe, ndc Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim wakati wa ziara ya Mhe. Balozi Battle ya kutembea kituo hicho.
Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mheshimiwa Michael Battle (aliyesimama) akitoa muhadhara wa kidiplomasia kwa baadhi ya wahadhiri na wanafunzi wa Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed.

Akiwa katika kituo hicho, Mheshimiwa Balozi Battle amekutana na kuzungumza na Dkt. Felix Wandwe, ndc Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Dkt. Salim Ahmed Salim, kutoa muhadhara wa kidiplomasia kwa baadhi ya wahadhiri na wanafunzi wa kituo pamoja na kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali aliyoulizwa na wanafunzi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news