Brigedia Jenerali Ndagala akagua eneo lililoathiriwa na maji ya mvua Kigamboni

DAR-Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu, Brigedia Jenerali Hosea Ndagala tarehe 9 Mei, 2024 amefanya ziara ya kutembelea Wilaya ya Kigamboni Kata ya Mjimwema katika Mtaa wa Maweni kwa lengo la kuangalia madhara yaliyotokea kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya nyumba zilizozingirwa na maji katika eneo la Mtaa wa Maweni Bondeni Kata ya Mji Mwema Wilaya ya Kigambini mkoa wa Dar es Salaam.
Mkurugenzi Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Brigedia Jenerali Hosea Ndagala akizungumza na katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu kabla ya kuanza ziara yake ya kukagua maeneo yaliyoathirika na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha Jijini Dar es Salaam kushoto kwake ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya menejimenti ya Maafa sehemu ya Operesheni, Luteni Kanali Selestine Masalamado.
Katibu Tawala Msaidizi (Mipango na Uratibu),Chillah Moses akitoa maelezo juu ya eneo la Mtaa wa Maweni kata ya Mji Mwema ambalo limezingirwa na maji yaliyotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika Jiji la Dar es Salaam.

Awali akiwa katika kikao cha pamoja na Katibu Tawala Msaidizi (Mipango na Uratibu) Ndg. Chillah Moses katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwaajili ya kupata taarifa kuhusu hali halisi ya madhara ya mvua hizo kwa Wilaya ya Kigamboni alielezwa kuwa maeneo yaliyoathiriwa ni pamoja na Mtaa wa Maweni eneo la Bondeni kata ya Mji Mwema pamoja na Maweni eneo la Biasi ambayo yamezingirwa na maji ya mvua zinazoendelea kunyesha Katika Mkoa huo.
Aidha, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu itaendelea kuratibu masuala ya menejimenti ya maafa nchini ili kuhakikisha jamii inaendelea kuwa salama na stahimilivu dhidi ya maafa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news