DCEA yafikisha elimu kuhusu madhara ya dawa za kulevya Bagamoyo

PWANI-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Pwani imeshirikiana na Asasi ya Life and Hope Rehabilitation kutoa elimu kuhusu madhara ya dawa kwa wanafunzi na walimu.

Ni wa Shule ya Sekondari Hassanali Dhamji iliyopo Bagamoyo, wavuvi na wachuuzi wa soko la samaki Bagamoyo.
Katika eneo la soko, elimu ilitolewa kwa kutumia kipaza sauti huku wachuuzi wakiendelea na biashara zao. Pia, waraibu wanaoendelea na tiba ya Methadone walitoa ushuhuda na kuwaasa vijana wasijiingize kwenye matumizi na biashara ya dawa za kulevya.

Mwenyekiti wa soko la hilo pamoja na waalimu wa shule ya Hassanali Dhamji wameomba elimu ya dawa za kulevya iwe endelevu katika maeneo yao.

#kataaDawazaKulevyaTimizaMalengoYako

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news