DODOMA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya (DCEA) Kanda ya Kati Dodoma imekabidhi silaha mbili za moto kwa RPC wa Dodoma zilizokamatwa kwenye operesheni zilizofanyika tarehe 24 hadi 28 Aprili,2024 mkoani humo.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, leo tarehe 3 Mei, 2024 katika ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Kaimu Kamishna Msaidizi Kanda ya Kati, Mzee Kasuwi amesema, silaha hizo aina ya gobore zilikuwa zinamilikiwa na Hamisi Chambo (46) na Abdilah Juma (45) wote wakazi wa Kata ya Segera na zilikuwa zikitumika kulinda mashamba ya bangi.


Tags
DCEA
DCEA Tanzania
Habari
Jeshi la Polisi Tanzania
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)