Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo Mei 16,2024

NJOMBE-Mkazi wa jijini Dar es Salaam amekamatwa na Polisi mkoani Njombe akiwa na shilingi milioni 29.4 katika nyumba ya kulala wageni ya Lisbon mjini Makambako, ambapo fedha hizo inadaiwa amezipora katika kampuni aliyokuwa anafanyia kazi ya Interchick jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Mahamoud Banga amesema, wamemkamata Mwakatundu wakiwa wanafanya upekuzi wa kawaida katika nyumba za kulala wageni ambapo baada ya mahojiano alikiri kupata fedha hizo kwa njia ya uporaji.

Banga amebainisha kuwa, tayari mtuhumiwa huyo amekabidhiwa kwa Jeshi la Polisi mkoani Dar es Salaam kwa hatua za kisheria.






















Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news