Mageuzi ya elimu Tanzania yatikisa Mkutano wa Elimu Duniani

LONDON-Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amewasilisha mada juu ya mageuzi ya Elimu Tanzania na kuwakosha wajumbe wa Mkutano wa Elimu Duniani unaofanyika jijini London, Uingereza.
Tanzania inashiriki katika mkutano huo ulioleta pamoja nchi zaidi ya 200 duniani kujadili maendeleo ya elimu duniani ikiwa ni nguzo kuu ya kuandaa rasilimali watu wenye ujuzi na mtaji mkubwa katika kuleta maendeleo.

Katika wasilisho, Prof. Mkenda ameelezea namna Tanzania ilivyoanza kazi ya utekelezaji mageuzi kwa kufanya mitaala kulenga elimu ujuzi na kusisitiza umuhimu wa wadau wa elimu wakajielekeza katika kutatua changamoto kimfumo ikiwemo ugharamiaji, vifaa, walimu bora na ujuzi.
Baada ya wasilisho hilo,Prof.Mkenda pia ameshiriki katika Jukwaa la Elimu kama mmoja wa wachangiaji kuhusu nini kifanyike kuwianisha elimu jumla na amali ili kuandaa wahitimu wataokidhi mazingira ya ajira na maisha ya kazi kwa ujumla.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news