Mkurugenzi Mkuu wa TEA ashiriki ufunguzi wa Maadhimisho ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu jijini Tanga

TANGA-Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA),Dkt. Erasmus Kipesha leo Mei 27, 2024 amehudhurua ufunguzi wa maadhimisho ya kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu katika viwanja vya shule ya sekondari Popatlal jijini Tanga.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA,Dkt. Erasmus Kipesha akiwa katika hafla ya uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Kitaifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu katika viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga.

Mgeni Rasmi wa ufunguzi wa maadhimisho hayo ya wiki moja ni Mhe. Prof. Adolf Mkenda (Mb) Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia.Mkurugenzi Mkuu wa TEA, Dkt. Erasmus Kipesha akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda hilo katika viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Utafutaji Rasilimali na Usimamizi wa Miradi wa TEA, Bw. Masozi Nyirenda.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA, Dkt. Erasmus Kipesha na Kaimu Mkurugenzi Utafutaji Rasilimali na Usimamizi wa Miradi,Bw. Masozi Nyirenda wakijadiliana jambo katika banda la TEA, kwenye Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga.

Maadhimisho haya yenye kauli mbiu ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu kwa Uchumi shindani yameanza Mei 25 na tamati rasmi itakuwa Mei 31, 2024.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA Dkt. Erasmus Kipesha na Kaimu Mkurugenzi Utafutaji Rasilimali na Usimamizi wa Miradi,Bw. Masozi Nyirenda wakifurahia jambo katika banda la TEA, kwenye maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal, Jijini Tanga. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano kwa Umma, Bi. Bestina Magutu.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA, Dkt. Erasmus Kipesha akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wanaoshiriki kwenye maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga.
Mkurugenzi Mkuu wa TEA, Dkt. Erasmus Kipesha akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanufaika wa ufadhili wa Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF) wanaoshiriki kwenye Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu yanayofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Popatlal jijini Tanga.

Awali, Dkt. Kipesha alitembelea banda la Mamlaka katika viwanja hivyo na kukutana baadhi ya wanufaika wa mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi kupitia ufadhili wa Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF) uliosimamiwa na TEA wakiwa na bidhaa zao wanazozalisha baada ya kupatiwa mafunzo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news