Nelson Memorial Secondary kinara kwa nidhamu na matokeo Mpwapwa mkoani Dodoma

DODOMA-Nelson Memorial Secondary School iliyopo wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma imeendelea kuwa kinara katika nidhamu na matokeo wilayani humo.
Pia, shule hiyo imeendelea kuwa kivutio kwa wazazi na walezi wengi kutokana na namna ambavyo imekuwa ikitoa huduma bora kuanzia elimu, malezi na maadili.
Kwa mujibu wa cheti cha pongezi kilichotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Nelson Memorial Secondary School katika matokeo ya kidato cha pili mwaka 2023 ilifanya vema zaidi na kufikia zaidi ya asilimia 100 ya lengo.

Cheti hicho kilichotolewa Februari 16, 2024 kimesainiwa na Afisa Elimu Sekondari wilayani humo, Benadetha Thomas na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri, Mwanahamisi H. Ally.
Shule hiyo ambayo ina usajili Na.S5879 ambayo ni ya bweni kwa wavulana na wasichana kipaumbele chao ni nidhamu na taaluma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news