Teknolojia mbadala kuimarisha mtandao wa barabara nchini

DAR-Teknolojia mbadala ya kuimarisha mtandao wa barabara ikiwemo ujenzi wa madaraja imara na madhubuti itaendelea kutumiwa nchini na Wakala wa Barabara za Vijijini na Vijijini (TARURA).
Hayo yameelezwa leo na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI,Mhandisi Rogatus Mativila mbele ya waandishi wa habari katika banda la maonesho ya TARURA kwenye mkutano wa 30 wa Wahandisi Washauri Afrika.

“TARURA wanaonesha utaalamu, wanafanya ikiwemo ujenzi wa ‘structure’ mbalimbali za kupitishia maji, wanajenga kwa mawe teknolojia ambayo inapunguza gharama,” amesema.
Akizungumza namna Serikali ilivyojipanga kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na mvua zilizoanza kunyesha tangu Oktoba, 2023 na zinazoendelea hadi sasa, Naibu Katibu Mkuu Mativila amebainisha kwamba bado kuna sehemu nyingi mvua zinaendelea kunyesha, miundombinu mingi imeharibika, mvua zilizokuja hazikuwa za kawaida kama miaka mingine.

Hata hivyo amesema,wameshafanya tathimini na zinahitaji kiasi cha shilingi bilioni 2 kurejeresha miundombinu iliyoharibiwa na mvua na Serikali ipo tayari kutoa fedha hizo

Naye msimamizi wa Teknolojia Mbadala TARURA Makao Makuu,Mhandisi Mshauri Pharels Ngeleja amesema,tayari wamejenga madaraja 256 kwa teknolojia ya mawe yaliyogharimu shilingi bilioni 13.
“Teknolojia ya mawe tunatumia pia kujenga barabara, kuna kilomita 28.18 zimekamilika mkoani Mwanza, Kigoma na Rukwa, pia kwenye barabara zetu zingine tunatumia teknolojia za Ecoroad, Ecozyme na Polymer.

“Tumejenga barabara ya Sawala kilomita 13 mkoani Iringa, Chamwino - Dodoma pia tunaendelea na hizi teknolojia, Dodoma kuna barabara inaitwa daraja dogo tumekamilisha.Miradi hii ipo maeneo mbalimbali ambapo tunaendelea,” amesema Mhandisi Ngereja.
Vilevile amesema,TARURA kupitia kitengo cha mambo ya mazingira wanaendelea pia kufuatilia kwa ukaribu athari za mabadiliko ya tabia nchi ili kujiimarisha zaidi katika ujenzi wa miundombinu yake.

TARURA imeweza kujenga barabara kwa kutumia teknolojia ya Ecoroad, Ecozyme na Polymer katika barabara ya Chamwino Km. 7,Itilima Km. 5, Sawala-Mkonge Km. 10 na Daraja dogo -Dodoma Km.1.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news