TFRA,Vodacom Tanzania wateta

DAR-Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), Joel Laurent na watendaji wake wamekutana katika kikao na maafisa watendaji wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom nchini ili kujadili mashirikiano baina ya mamlaka na kampuni hiyo ya simu.
Majadiliano hayo yamelenga kufanya tathmini ya ushiriki wao katika utekelezaji wa mpango wa ruzuku kwa msimu wa kilimo wa 2023/2024 tunapoelekea mwishoni kwa msimu wa kilimo.

Kampuni ya Vodacom imeonesha utayari wake kuendelea kushirikiana na mamlaka katika nyaja ya mafunzo ya matumizi ya vishikwambi kwa maafisa ugani wakati wa zoezi la usajili wa wakulima na mafunzo ya utoaji huduma kwa wateja wa mbolea kwa msimu ujao wa kilimo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news