Tuache tabia ya kuwanyanyapaa wagonjwa wa Afya ya Akili-Waziri Ummy

DODOMA-Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amewataka wananchi kuacha tabia ya kuwanyanyapaa wagonjwa wa Afya Akili pamoja na na kuwahi kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya mapema.
Waziri Ummy amesema hayo bungeni Mei 13, 2024 akiwa anawasilisha hotuba yake ya bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2024/25 akielezea utekelezaji wa majukumu ya Wizara katika utoaji wa huduma za Kinga nchini.

"Natoa wito kwa Watanzania kuacha kuwanyanyapaa wagonjwa wa akili na kuwahi kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa ajili ya uchunguzi na matibabu ya mapema,"amesema Waziri Ummy.

Aidha, Waziri Ummy amesema Wizara imeendelea kuimarisha huduma za Afya ya Akili kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ambapo inakamilisha mkakati wa utoaji wa huduma za Afya ya Akili na msaada wa kisaikolojia kwa kijamii.

"Magonjwa ya akili yanajumuisha magonjwa yanayotokana na Matumizi ya Dawa za kulevya, Psychoses, kifafa na Neuroses,"amesema Waziri Ummy.

Katika kipindi cha Julai, 2023 hadi Machi 2024 Waziri Ummy amesema, waliohudhuria kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwa shida ya magonjwa ya afya ya Akili walikuwa 293,952 sawa na 6.3% ya wagonjwa wa magonjwa yasiyoambukiza ikilinganishwa na 246,544 sawa na asilimia 6 kwa kipindi cha mwaka 2022/23.

"Kwa wagonjwa waliolazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya wenye magonjwa ya afya ya Akili walikuwa 19,506 sawa na 7% ya wagonjwa wa magonjwa yasiyoambukiza ikilinganishwa na wagonjwa 13,262 sawa na 5% katika kipindi cha mwaka 2022/23,"amesema Waziri Ummy.

Ongezeko hili la wagonjwa wa afya ya akili limetokana na kuongezeka kwa uelewa wa jamii kuhusu magonjwa haya na kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news