NA GODFREY NNKO
SERIKALI kupitia Wizara ya Fedha imesema, wadau wa sekta ya habari ni nguzo muhimu katika kuchochea maendeleo ya uchumi nchini.
.jpg)
"Wadau katika sekta ya habari wapo katika nafasi kubwa katika kuchochea maendeleo ya uchumi wetu kwa njia ya kuwahamasisha wananchi kutekeleza kwa pamoja malengo ya Taifa.
"Kwa sababu, wadau kutoka sekta ya habari wataandika na kutangaza taarifa za mipango ya maendeleo, utekelezaji wa mipango ya maendeleo na mrejesho kutoka kwa wanachi juu ya mapokeo ya mipango ya maendeleo,"amesisitiza Bi.Kingdom.
Pia, amesema ni vema wadau wa sekta ya habari kuendelea kushirikiana na sekta ya umma katika kuleta maendeleo nchini.
Mbali na hayo, Mchumi Mkuu huyo ametaja vipaumbele vitano katika utekelezaji wa bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Vile vile kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea maendeleo ya watu,kuendeleza rasilimali watu na kuchochea uchumi shindani na shirikishi nchini.
Bi.Kingdom amesema, ili kuweza kufanikisha vipaumbele hivyo,Serikali inajielekeza zaidi katika kuongeza mikakati ya ukusanyaji wa mapato ambayo yatatumika kugharamia miradi ya maendeleo nchini.
Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na hamasa ya kuwahimiza wananchi kila wanapofanya manunuzi ya bidhaa kuhakikisha wanadai risti halali za kieletroniki kulingana na kiasi alicholipia.
Amesema, ili kufikia malengo hayo, vyombo vya habari vinategemewa kuwa daraja muhimu kati ya Serikali na wananchi ili waweze kushiki kikamilifu kulipa kodi ambazo zitawezesha Serikali kufikia malengo.
Amesema, kupitia vyombo vya habari wananchi wanahitaji kusikia mambo gani yamefanyika kupitia kodi zao.

Amesema, kutokana na asilimia 70 ya bajeti kutegemea mapato ya ndani nchini, kila mwananchi ana nafasi kubwa kufanikisha upatikanaji wa mapato hayo.

Mchumi Mkuu amesema,mapato ya nje ni yale yanayotokana na mikopo nafuu na mikopo ya kibiashara ikiwemo misaada ya washirika wa maendeleo.