Afisa Mtendaji wa Kata ya Iwindi,wenzake watiwa hatiani

MBEYA-Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mbeya imewahukumu Afisa Mtendaji wa Kata ya Iwindi na wenzake wawili kulipa faini ya shilingi 500,000 kila mmoja au kwenda jela miaka mitatu.
Ni kwa kosa la kupokea rushwa kiasi cha sh. 130,000 kinyume na kifungu cha 15(1)(a) na (2) cha sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11/2007.

Hukumu hiyo dhidi ya Bw. Rubaha Mkwekwele Sonje, Bw.Alex lauden Chawe na Bi.Lenisa Raphael Simon katika shauri la jinai Na. 09/2023, ilitolewa Juni 10, 2024 na Hakimu Mkazi Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya, Mhe. Scout Peter Andrew.

Washtakiwa walifikishwa kizimbani kwa shtaka la kupokea rushwa kiasi cha sh. 130,000 toka kwa mwananchi ili waweze kumpatia barua ya utambulisho wa kumdhamini ndugu yake aliyekuwa anashikiliwa Kituo cha Polisi Mbalizi.

Hata hivyo, washtakiwa wamelipa faini na kuachiwa huru.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news